scripture.how 聖書写経
JA

Copywork

Swahili 1850 Luke 1장

写経は速く終える入力練習ではなく、一節ずつみ言葉の文と流れを改めて受け止める時間です。入力内容はこのブラウザに一時保存され、ログインするとアカウントにも保存されます。

KO 韓国語
ZH 中国語
JA 日本語
HI ヒンディー語
BN ベンガル語
TA タミル語
TE テルグ語
ML マラヤーラム語
FA ペルシア語
MY ビルマ語
NE ネパール語
MR マラーティー語
KN カンナダ語
HA ハウサ語
YO ヨルバ語
SW スワヒリ語
IG イボ語
ID インドネシア語
TSI
PT ポルトガル語
VI ベトナム語
AR アラビア語
AVD
RU ロシア語
UK ウクライナ語
RO ルーマニア語
BTF
IT イタリア語
FI フィンランド語
TO トンガ語
HR クロアチア語
SR セルビア語
TR トルコ語
HU ハンガリー語
PL ポーランド語
SK スロバキア語
LA ラテン語
NL オランダ語
CS チェコ語
FR フランス語
ES スペイン語
DE ドイツ語
ETC その他の言語

小見出し単位で進める · Luke

1:1-4 Dedication to Theophilus 1:5-25 The Birth of John the Baptist Foretold 1:26-38 The Birth of Jesus Foretold 1:39-45 Mary Visits Elizabeth 1:46-56 Mary's Song of Praise: The Magnificat 1:57-66 The Birth of John the Baptist 1:67-80 Zechariah's Prophecy 2:1-7 The Birth of Jesus in Bethlehem 2:8-20 The Shepherds and the Angels 2:21-24 Jesus Presented in the Temple 2:25-35 Simeon Holds the Child 2:36-40 The Testimony of the Prophetess Anna 2:41-52 The Boy Jesus in the Temple 3:1-14 John the Baptist Prepares the Way 3:15-17 The Testimony of John the Baptist 3:18-20 John the Baptist Imprisoned 3:21-22 The Baptism of Jesus 3:23-38 The Genealogy of Jesus 4:1-13 The Temptation of Jesus 4:14-30 Jesus Rejected at Nazareth 4:31-37 Jesus Drives Out an Unclean Spirit 4:38-39 Jesus Heals Peter's Mother-in-Law 4:40-44 Jesus Heals Many and Withdraws to Pray 5:1-11 The Miraculous Catch of Fish 5:12-16 Jesus Cleanses a Leper 5:17-26 Jesus Heals a Paralytic 5:27-32 Jesus Calls Levi the Tax Collector 5:33-39 The Question About Fasting and New Wine 6:1-5 Jesus Is Lord of the Sabbath 6:6-11 Jesus Heals a Man with a Withered Hand on the Sabbath 6:12-16 Jesus Chooses the Twelve Apostles 6:17-26 Blessings and Woes on the Plain 6:27-36 Love Your Enemies 6:37-42 Do Not Judge 6:43-45 A Tree Is Known by Its Fruit 6:46-49 The House Built on the Rock 7:1-10 The Faith of the Centurion 7:11-17 Jesus Raises the Widow's Son at Nain 7:18-35 The Question of John the Baptist 7:36-50 A Sinful Woman's Love and Forgiveness 8:1-3 The Women Who Served Jesus 8:4-8 The Parable of the Sower 8:9-15 The Parable of the Sower Explained 8:16-18 A Lamp on a Stand 8:19-21 Jesus' True Family 8:22-25 Jesus Calms the Storm 8:26-39 Jesus Heals a Demon-Possessed Man at Gerasa 8:40-56 Jairus's Daughter and the Woman with the Issue of Blood 9:1-6 Jesus Sends Out the Twelve 9:7-9 Herod Hears About Jesus 9:10-17 Jesus Feeds the Five Thousand 9:18-21 Peter's Confession of Faith 9:22-27 Jesus Foretells His Suffering 9:28-36 The Transfiguration 9:37-43 Jesus Heals a Boy with an Unclean Spirit 9:44-45 Jesus Again Foretells His Death 9:46-50 Who Is the Greatest 9:51-56 A Samaritan Village Rejects Jesus 9:57-62 The Cost of Following Jesus 10:1-12 Jesus Sends Out the Seventy-Two 10:13-16 Woes on Unrepentant Towns 10:17-20 The Return of the Seventy-Two 10:21-24 Jesus Rejoices and Gives Thanks 10:25-37 The Parable of the Good Samaritan 10:38-42 Martha and Mary 11:1-13 Jesus Teaches on Prayer 11:14-23 Jesus and Beelzebul 11:24-28 The Generation That Seeks a Sign 11:29-32 The Sign of Jonah 11:33-36 The Lamp of the Body Is the Eye 11:37-54 Woes to the Pharisees and Lawyers 12:1-12 Beware of the Leaven of the Pharisees 12:13-21 The Parable of the Rich Fool 12:22-34 Do Not Be Anxious About Your Life 12:35-48 Watchful Servants 12:49-53 Jesus Came to Bring Division 12:54-59 Interpreting the Present Time 13:1-5 Repent or Perish 13:6-9 The Parable of the Barren Fig Tree 13:10-17 Jesus Heals a Crippled Woman on the Sabbath 13:18-19 The Parable of the Mustard Seed 13:20-21 The Parable of the Leaven 13:22-30 The Narrow Door 13:31-35 Lament Over Jerusalem 14:1-6 Jesus Heals a Man with Dropsy on the Sabbath 14:7-14 The Lesson of the Lowest Place 14:15-24 The Parable of the Great Banquet 14:25-35 The Cost of Discipleship 15:1-7 The Parable of the Lost Sheep 15:8-10 The Parable of the Lost Coin 15:11-32 The Parable of the Lost Son 16:1-13 The Parable of the Dishonest Manager 16:14-18 The Law and the Kingdom of God 16:19-31 The Rich Man and Lazarus 17:1-4 On Temptations to Sin and Forgiveness 17:5-10 Faith Like a Mustard Seed and the Servant's Duty 17:11-19 Jesus Cleanses Ten Lepers 17:20-37 The Coming of the Kingdom of God 18:1-8 The Parable of the Persistent Widow and the Unjust Judge 18:9-14 The Pharisee and the Tax Collector 18:15-17 Jesus Blesses the Little Children 18:18-30 The Rich Ruler 18:31-34 Jesus Foretells His Death a Third Time 18:35-43 Jesus Heals a Blind Beggar at Jericho 19:1-10 Jesus Calls Zacchaeus the Tax Collector 19:11-27 The Parable of the Ten Minas 19:28-40 The Triumphal Entry into Jerusalem 19:41-44 Jesus Weeps Over Jerusalem 19:45-48 Jesus Cleanses the Temple 20:1-8 The Authority of Jesus Questioned 20:9-19 The Parable of the Tenants 20:20-26 Paying Taxes to Caesar 20:27-40 The Question About the Resurrection 20:41-44 Whose Son Is the Christ 20:45-47 Beware of the Scribes 21:1-4 The Widow's Two Coins 21:5-36 The Olivet Discourse: Signs of the End 22:1-6 Judas Plots to Betray Jesus 22:7-13 Preparation of the Passover 22:14-20 The Institution of the Lord's Supper 22:21-23 Jesus Foretells His Betrayal 22:24-30 The Dispute About Who Is the Greatest 22:31-34 Jesus Foretells Peter's Denial 22:35-38 Purse, Bag, and Sword 22:39-46 Jesus Prays on the Mount of Olives 22:47-53 The Betrayal and Arrest of Jesus 22:54-62 Peter Denies Jesus 22:63-71 Jesus Before the Council 23:1-25 Jesus Before Pilate 23:26-43 The Crucifixion 23:44-49 The Death of Jesus 23:50-56 The Burial of Jesus 24:1-12 The Resurrection 24:13-35 On the Road to Emmaus 24:36-49 Jesus Appears to His Disciples 24:50-53 The Ascension
1:1
待機

Mheshimiwa Theofilo: Watu wengi wamejitahidi kuandika juu ya mambo yale yaliyotendeka kati yetu.

1:2
待機

Waliandika kama tulivyoelezwa na wale walioyaona kwa macho yao tangu mwanzo, na waliotangaza ujumbe huo.

1:3
待機

Inafaa nami pia, Mheshimiwa, baada ya kuchunguza kwa makini mambo yote tangu mwanzo, nikuandikie kwa mpango,

1:4
待機

ili nawe uweze kujionea mwenyewe ukweli wa mambo yale uliyofundishwa.

1:5
待機

Wakati Herode alipokuwa mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani mmoja jina lake Zakaria, wa kikundi cha Abia. Mke wake alikuwa anaitwa Elisabeti, naye alikuwa wa ukoo wa kuhani Aroni.

1:6
待機

Wote wawili walikuwa wanyofu mbele ya Mungu, wakiishi kwa kufuata amri na maagizo yote ya Bwana bila lawama.

1:7
待機

Lakini hawakuwa wamejaliwa watoto kwa vile Elisabeti alikuwa tasa, nao wote wawili walikuwa wazee sana.

1:8
待機

Siku moja, ilipokuwa zamu yake ya kutoa huduma ya ukuhani mbele ya Mungu,

1:9
待機

Zakariya alichaguliwa kwa kura, kama ilivyokuwa desturi, kuingia hekaluni ili afukize ubani.

1:10
待機

Watu, umati mkubwa, walikuwa wamekusanyika nje wanasali wakati huo wa kufukiza ubani.

1:11
待機

Malaika wa Bwana akamtokea humo ndani, akasimama upande wa kulia wa madhabahu ya kufukizia ubani.

1:12
待機

Zakariya alipomwona alifadhaika, hofu ikamwingia.

1:13
待機

Lakini malaika akamwambia, “Zakariya, usiogope, kwa maana sala yako imesikilizwa, na Elisabeti mkeo atakuzalia mtoto wa kiume, nawe utampa jina Yohane.

1:14
待機

Utakuwa na furaha kubwa na watu wengi watashangilia kwa sababu ya kuzaliwa kwake.

1:15
待機

Atakuwa mkuu mbele ya Bwana. Hatakunywa divai wala kileo, atajazwa Roho Mtakatifu tangu tumboni mwa mama yake.

1:16
待機

Atawaelekeza wengi wa watu wa Israeli kwa Bwana Mungu wao.

1:17
待機

Atamtangulia Bwana akiongozwa na nguvu na roho kama Eliya. Atawapatanisha kina baba na watoto wao; atawafanya wasiotii wawe na fikira za uadilifu, na hivyo amtayarishie Bwana watu wake.”

1:18
待機

Zakariya akamwambia huyo malaika, “Ni kitu gani kitakachonihakikishia jambo hilo? Mimi ni mzee, hali kadhalika na mke wangu.”

1:19
待機

Malaika akamjibu, “Mimi ni Gabrieli, nisimamaye mbele ya Mungu, na nimetumwa niseme nawe, nikuletee hii habari njema.

1:20
待機

Sikiliza, utakuwa bubu kwa sababu huyasadiki haya maneno yatakayotimia kwa wakati wake. Hutaweza kusema mpaka hayo niliyokuambia yatakapotimia.”

1:21
待機

Wakati huo, wale watu walikuwa wanamngoja Zakariya huku wakishangaa juu ya kukawia kwake Hekaluni.

1:22
待機

Alipotoka nje, hakuweza kusema nao. Ikawa dhahiri kwao kwamba alikuwa ameona maono Hekaluni. Lakini akawa anawapa ishara kwa mikono, akabaki bubu.

1:23
待機

Zamu yake ya kuhudumu ilipokwisha, alirudi nyumbani.

1:24
待機

Baadaye Elisabeti mkewe akapata mimba. Akajificha nyumbani kwa muda wa miezi mitano, akisema:

1:25
待機

“Hivi ndivyo alivyonitendea Bwana; ameniangalia na kuniondolea aibu niliyokuwa nayo mbele ya watu.”

1:26
待機

Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya,

1:27
待機

kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi.

1:28
待機

Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.”

1:29
待機

Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini?

1:30
待機

Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema.

1:31
待機

Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu.

1:32
待機

Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake.

1:33
待機

Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.”

1:34
待機

Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?”

1:35
待機

Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu.

1:36
待機

Ujue pia kwamba hata Elisabeti, jamaa yako, naye amepata mimba ingawa ni mzee, na sasa ni mwezi wa sita kwake yeye ambaye watu walimfahamu kuwa tasa.

1:37
待機

Kwa maana hakuna jambo lisilowezekana kwa Mungu.”

1:38
待機

Maria akasema, “Mimi ni mtumishi wa Bwana, nitendewe kama ulivyosema.” Kisha yule malaika akaenda zake.

1:39
待機

Siku kadhaa baadaye, Maria alifunga safari akaenda kwa haraka hadi mji mmoja ulioko katika milima ya Yuda.

1:40
待機

Huko, aliingia katika nyumba ya Zakariya, akamsalimu Elisabeti.

1:41
待機

Mara tu Elisabeti aliposikia sauti ya Maria, mtoto mchanga tumboni mwake Elisabeti akaruka. Naye Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifiu,

1:42
待機

akasema kwa sauti kubwa, “Umebarikiwa kuliko wanawake wote, naye utakayemzaa amebarikiwa.

1:43
待機

Mimi ni nani hata mama wa Bwana wangu afike kwangu?

1:44
待機

Nakwambia, mara tu niliposikia sauti yako, mtoto mchanga tumboni mwangu aliruka kwa furaha.

1:45
待機

Heri yako wewe uliyesadiki kwamba yatatimia yale Bwana aliyokwambia.”

1:46
待機

Naye Maria akasema,

1:47
待機

“Moyo wangu wamtukuza Bwana, roho yangu inafurahi kwa sababu ya Mungu Mwokozi wangu.

1:48
待機

Kwa kuwa amemwangalia kwa huruma mtumishi wake mnyenyekevu. Hivyo tangu sasa watu wote wataniita mwenye heri.

1:49
待機

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu amenitendea makuu, jina lake ni takatifu.

1:50
待機

Huruma yake kwa watu wanaomcha hudumu kizazi hata kizazi.

1:51
待機

Amefanya mambo makuu kwa mkono wake: amewatawanya wenye kiburi katika mawazo ya mioyo yao;

1:52
待機

amewashusha wenye nguvu kutoka vitu vyao vya enzi, akawakweza wanyenyekevu.

1:53
待機

Wenye njaa amewashibisha mema, matajiri amewaacha waende mikono mitupu.

1:54
待機

Amemsaidia Israeli mtumishi wake, akikumbuka huruma yake.

1:55
待機

Kama alivyowaahidia wazee wetu Abrahamu na wazawa wake hata milele.”

1:56
待機

Maria alikaa na Elisabeti kwa muda upatao miezi mitatu, halafu akarudi nyumbani kwake.

1:57
待機

Wakati wa kujifungua kwake Elisabeti ulifika, akajifungua mtoto wa kiume.

1:58
待機

Jirani na watu wa jamaa yake walipopata habari kwamba Bwana amemwonea huruma kubwa, walifurahi pamoja naye.

1:59
待機

Halafu siku ya nane walifika kumtahiri mtoto, wakataka kumpa jina la baba yake, Zakariya.

1:60
待機

Lakini mama yake akasema, “La, sivyo, bali ataitwa Yohane.”

1:61
待機

Wakamwambia, “Mbona hakuna yeyote katika ukoo wake mwenye jina hilo?”

1:62
待機

Basi, wakamwashiria baba yake wapate kujua alitaka mtoto wake apewe jina gani.

1:63
待機

Naye akaomba kibao cha kuandikia, akaandika hivi: “Yohane ndilo jina lake.” Wote wakastaajabu.

1:64
待機

Papo hapo midomo na ulimi wake Zakariya vikafunguliwa, akawa anaongea akimsifu Mungu.

1:65
待機

Hofu ikawaingia jirani wote, na habari hizo zikaenea kila mahali katika milima ya Yudea.

1:66
待機

Wote waliosikia mambo hayo waliyatafakari mioyoni mwao wakisema: “Mtoto huyu atakuwa mtu wa namna gani?” Maana, hakika nguvu ya Bwana ilikuwa pamoja naye.

1:67
待機

Zakariya, baba yake mtoto, akajazwa Roho Mtakatifu, akatamka ujumbe wa Mungu:

1:68
待機

“Asifiwe Bwana Mungu wa Israeli, kwani amekuja kuwasaidia na kuwakomboa watu wake.

1:69
待機

Ametupatia Mwokozi shujaa, mzawa wa Daudi mtumishi wake.

1:70
待機

Aliahidi hapo kale kwa njia ya manabii wake watakatifu,

1:71
待機

kwamba atatuokoa mikononi mwa adui zetu na kutoka mikononi mwa wote wanaotuchukia.

1:72
待機

Alisema atawahurumia wazee wetu, na kukumbuka agano lake takatifu.

1:73
待機

Kiapo alichomwapia Abrahamu baba yetu, ni kwamba atatujalia sisi

1:74
待機

tukombolewe kutoka adui zetu, tupate kumtumikia bila hofu,

1:75
待機

kwa unyofu na uadilifu mbele yake, siku zote za maisha yetu.

1:76
待機

Nawe mwanangu, utaitwa, nabii wa Mungu Mkuu, utamtangulia Bwana kumtayarishia njia yake;

1:77
待機

kuwatangazia watu kwamba wataokolewa kwa kuondolewa dhambi zao.

1:78
待機

Mungu wetu ni mpole na mwenye huruma. Atasababisha pambazuko angavu la ukombozi litujie kutoka juu,

1:79
待機

na kuwaangazia wote wanaokaa katika giza kuu la kifo, aongoze hatua zetu katika njia ya amani.”

1:80
待機

Mtoto akakua, akapata nguvu rohoni. Alikaa jangwani mpaka alipojionyesha rasmi kwa watu wa Israeli.