scripture.how 성경필사
KO

Copywork

Swahili 1850 요한계시록 2장

성경필사는 빠르게 끝내는 입력 훈련이 아니라, 한 절씩 말씀의 문장과 흐름을 다시 붙드는 시간입니다. 입력 내용은 이 브라우저에 임시 저장되며, 로그인하면 계정에도 저장됩니다.

KO 한국어
ZH 중국어
JA 일본어
HI 힌디어
BN 벵골어
TA 타밀어
TE 텔루구어
ML 말라얄람어
FA 페르시아어
MY 버마어
NE 네팔어
MR 마라티어
KN 칸나다어
HA 하우사어
YO 요루바어
SW 스와힐리어
IG 이그보어
ID 인도네시아어
TSI
PT 포르투갈어
VI 베트남어
AR 아랍어
AVD
RU 러시아어
UK 우크라이나어
RO 루마니아어
BTF
IT 이탈리아어
FI 핀란드어
TO 통가어
HR 크로아티아어
SR 세르비아어
TR 튀르키예어
HU 헝가리어
PL 폴란드어
SK 슬로바키아어
LA 라틴어
NL 네덜란드어
CS 체코어
FR 프랑스어
ES 스페인어
DE 독일어
ETC 기타 언어

소제목 단위로 진행 · 요한계시록

1:1-3 The Prologue and the Blessing on the Reader 1:4-8 Greetings and Doxology to the Seven Churches 1:9-20 The Vision of One Like a Son of Man on Patmos 2:1-7 To the Church in Ephesus: You Have Forsaken Your First Love 2:8-11 To the Church in Smyrna: Be Faithful in Tribulation 2:12-17 To the Church in Pergamum: Tolerating False Teaching 2:18-29 To the Church in Thyatira: Following Jezebel 3:1-6 To the Church in Sardis: Alive in Name but Dead 3:7-13 To the Church in Philadelphia: Given an Open Door 3:14-22 To the Church in Laodicea: Lukewarm and Spit Out 4:1-6 The Throne in Heaven and Its Surrounding Glory 4:7-11 The Worship of the Four Living Creatures and Twenty-Four Elders 5:1-5 The Sealed Scroll and the Search for One Worthy 5:6-10 The Slain Lamb Who Takes the Scroll 5:11-14 The Praise of All Creation 6:1-8 The Four Horses and Their Riders from the Seals 6:9-11 The Cry of the Martyrs Under the Altar 6:12-17 The Sixth Seal and the Great Day of Wrath 7:1-8 The 144,000 of Israel Who Are Sealed 7:9-17 The Great Multitude in White from Every Nation 8:1-6 The Seventh Seal and the Preparation of the Seven Trumpets 8:7-13 The Plagues of the First Four Trumpets 9:1-12 The Fifth Trumpet and the Locusts from the Abyss 9:13-21 The Sixth Trumpet and the Deadly Cavalry 10:1-7 The Mighty Angel with the Little Scroll 10:8-11 The Command to Take and Eat the Little Scroll 11:1-14 The Ministry, Death, and Resurrection of the Two Witnesses 11:15-19 The Seventh Trumpet and the Praise in Heaven 12:1-6 The Woman Clothed with the Sun and the Red Dragon 12:7-12 The Dragon and His Army Cast Out of Heaven 12:13-17 The Fury of the Dragon Persecuting the Woman 13:1-10 The Beast Rising Out of the Sea 13:11-18 The Beast Out of the Earth and Its Number 14:1-5 The Lamb and the 144,000 on Mount Zion 14:6-13 The Cry of the Three Angels and the Blessed Dead 14:14-20 The Harvest of the Earth and the Winepress of Wrath 15:1-4 The Last Plagues and the Song of the Victors 15:5-8 The Angels Given the Seven Bowls of Wrath 16:1-11 The Plagues of the First Five Bowls 16:12-16 The Sixth Bowl and the Gathering at Armageddon 16:17-21 The Seventh Bowl and the Fall of the Great City 17:1-6 The Vision of the Great Prostitute on the Beast 17:7-18 The Interpretation of the Mystery of the Beast and the Prostitute 18:1-8 The Declaration of the Fall of Babylon the Great 18:9-20 Those Who Mourn the Fall of Babylon 18:21-24 The End of the City Thrown Down Like a Millstone 19:1-10 The Praise in Heaven and the Marriage Supper of the Lamb 19:11-16 The Rider on the White Horse, Faithful and True 19:17-21 The Defeat of the Beast and the False Prophet 20:1-6 The Dragon Bound a Thousand Years and the Reign of the Saints 20:7-10 The Final Defeat of the Released Satan 20:11-15 The Judgment at the Great White Throne and the Book of Life 21:1-8 The New Heaven, the New Earth, and the New Jerusalem 21:9-21 The Glory of the Holy City and Its Design 21:22-27 The City with No Temple, Filled with Light 22:1-5 The River of the Water of Life and the Tree of Life 22:6-15 The Promise of Coming Soon and the Warning 22:16-21 The Final Testimony and the Plea for the Lord
2:1
대기

“Kwa malaika wa kanisa la Efeso andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye ashikaye nyota saba katika mkono wake wa kulia, na ambaye hutembea katikati ya vinara saba vya taa vya dhahabu.

2:2
대기

Najua mambo yako yote; najua bidii yako na uvumilivu wako. Najua kwamba huwezi kuwavumilia watu waovu, na kwamba umewapima wale wanaojisemea kuwa mitume na kumbe sio, ukagundua kwamba ni waongo.

2:3
대기

Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.

2:4
대기

Lakini ninayo hoja moja juu yako: wewe hunipendi tena sasa kama pale awali.

2:5
대기

Basi, pakumbuke pale ulipokuwa kabla ya kuanguka, ukayaache madhambi yako, na kufanya kama ulivyofanya pale awali. La sivyo, naja kwako na kukiondoa kinara chako mahali pake.

2:6
대기

Lakini nakusifu juu ya kitu kimoja: wewe unayachukia wanayoyatenda Wanikolai kama ninavyoyachukia mimi.

2:7
대기

“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa haki ya kula matunda ya mti wa uzima ulioko ndani ya bustani ya Mungu.

2:8
대기

“Kwa malaika wa kanisa la Smurna andika hivi: “Huu ndio ujumbe kutoka kwake yeye wa kwanza na wa mwisho, ambaye alikufa na akaishi tena.

2:9
대기

Najua taabu zako; najua pia umaskini wako, ingawaje kwa kweli wewe ni tajiri; najua kashfa walizokufanyia wale wanaojiita Wayahudi lakini si Wayahudi wa kweli, bali ni kundi lake Shetani.

2:10
대기

Usiogope hata kidogo yale ambayo itakulazimu kuteseka. Sikiliza! Ibilisi anataka kuwajaribu kwa kuwatia baadhi yenu gerezani; nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Muwe waaminifu hata mpaka kufa, nami nitawapeni taji ya uzima.

2:11
대기

“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda hawataumizwa na kifo cha pili.

2:12
대기

“Kwa malaika wa kanisa la Pergamoni andika hivi: “Huu ndio ujumbe wake yeye aliye na upanga mkali wenye kuwili.

2:13
대기

Najua unakoishi: Wewe unaishi kwenye makao makuu ya Shetani! Lakini bado unashikilia jina langu; hukuikana imani yako kwangu hata siku zile Antipa shahidi wangu mwaminifu, alipouawa pale mahali anapoishi Shetani.

2:14
대기

Lakini ninayo machache dhidi yako: baadhi yenu ni wafuasi wa Balaamu aliyemfundisha Balaki kuwatega wana wa Israeli wale vyakula vilivyotambikiwa sanamu za kufanya uzinzi.

2:15
대기

Vivyo hivyo, wako pia miongoni mwenu watu wanaofuata mafundisho ya Wanikolai.

2:16
대기

Basi, achana na madhambi yako. La sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga utokao kinywani mwangu.

2:17
대기

“Aliye na masikio, basi, na asikie yale Roho anayoyaambia makanisa! “Wale wanaoshinda nitawapa ile mana iliyofichika. Nitawapa pia jiwe jeupe lililoandikwa jina jipya ambalo hakuna mtu aliyelijua isipokuwa tu wale wanaolipokea.

2:18
대기

“Kwa malaika wa kanisa la Thuatira andika hivi: “Huu ndio ujumbe wa Mwana wa Mungu, ambaye macho yake yametameta kama moto, na miguu yake inang'aa kama shaba iliyosuguliwa.

2:19
대기

Najua mambo yako yote. Najua upendo wako, imani yako, utumishi wako na uvumilivu wako. Wewe unafanya vizuri zaidi sasa kuliko pale awali.

2:20
대기

Lakini nina hoja moja juu yako: wewe unamvumilia yule mwanamke Yezabeli anayejiita nabii wa Mungu. Yeye huwafundisha na kuwapotosha watumishi wangu wafanye uzinzi na kula vyakula vilivyotambikiwa sanamu.

2:21
대기

Nimempa muda wa kutubu dhambi zake, lakini hataki kuachana na uzinzi wake.

2:22
대기

Sikiliza! Sasa namtupa kitandani ambapo yeye pamoja na wote waliofanya uzinzi naye watapatwa na mateso makali. Naam, nitafanya hivyo, kama wasipotubu matendo yao mabaya waliyotenda naye.

2:23
대기

Tena nitawaua wafuasi wake, ili makanisa yote yatambue kwamba mimi ndiye ninayechunguza mioyo na fikira za watu.

2:24
대기

“Lakini ninyi wengine mlioko huko Thuatira ambao hamfuati mafundisho yake Yezabeli, na ambao hamkujifunza kile wanachokiita Siri ya Shetani, nawaambieni kwamba sitawapeni mzigo mwingine.

2:25
대기

Lazima mzingatie yale mliyo nayo sasa mpaka nitakapokuja.

2:26
대기

“Wanaoshinda, na wale watakaozingatia mpaka mwisho kutenda ninayotaka, nitawapa mamlaka juu ya mataifa.

2:27
대기

Naam, nitawapa uwezo uleule nilioupokea kwa Baba: yaani, watayatawala mataifa kwa fimbo ya chuma na kuyavunjavunja kama chombo cha udongo.

2:28
대기

Tena nitawapa nyota ya asubuhi.

2:29
대기

“Aliye na masikio, basi, na ayasikie yale Roho anayoyaambia makanisa!